Thursday, June 23, 2022

Maswali ya vitabu na majibu yake

 NECTA 2012

“Washairi ni wataalamu wazuri na waliobobea katika kutumia taswira zinazotoa ujumbe kwa jamii.” Tumia taswira tatu kwa kila diwani kati ya diwani mbili zilizoorodheshwa kuthibitisha kauli hiyo. 

Utangulizi

Ni kweli kuwa washairi ni wataalamu wazuri na waliobobea katika kutumia taswira zinazotoa ujumbe kwa jamii.Ninathibitisha kwa kutumia diwani mbili ambazo ni diwani ya WASAKATONGE na diwani ya MALENGA WAPYA. Nikianza na diwani ya WASAKATONGE kama ifuatavyo;

Diwani ya wasakatonge  

Taswira ya Vinyonga- Ujumbe "Viongozi wasaliti mwenye tabia ya kigeugeu. Katika shairi la VINYONGA.

Taswira ya Miamba - Ujumbe " Watu mwenye mamlaka /watu wa tabaka la juu au wenye dhamana. Katika shairi la MIAMBA.

Taswira ya Bundi - Ujumbe " wakoloni mamboleo" katika shairi la BUNDI.

Taswira ya Jiko - Ujumbe " Mwanamke asiyejitunza na kujieheshimu yaani Malaya . katika shairi la WEWE JIKO LA SHAMBA.

Taswira ya Wasakatonge - Ujumbe " Watu wa Tabaka la chini ( Masikini) katika Shairi la WASAKATONGE.

Taswira ya Tonge la ugali - Ujumbe " Malighafi" katika shairi la Tonge la Ugali.

DIWANI YA MALENGA WAPYA

Taswira ya njiwa - Ujumbe  " Mpenzi " Shairi la NIPATE WAPI MWINGINE?

Taswira ya Punda - Ujumbe " tabaka linalokandamizwa " shairi la PUNDA.

Taswira la UA - Ujumbe " Mwanamke" Shairi la UA.

Taswira ya Samaki - Ujumbe " Tabaka tawaliwa au mwanachi wa tabaka la chini" Shairi la SAMAKI MTUNGONI.

Taswira ya Mvuvi - Ujumbe " Ni watu wa tabaka la juu (viongozi ) shairi la SAMAKI MTUNGONI.

Taswira ya MTUNGO - Ujumbe " Ni sheria ,kanuni au taratibu zinazotumiwa kuwabana watu wa tabaka la chini. Shairi la SAMAKI MTUNGONI

Tumia vitabu viwili vya riwaya kati ya vilivyoorodheshwa, kutoa hoja tatu kwa kila kitabu, zinazothibitisha dai kuwa mwanaume ni kikwazo cha mafanikio katika jamii.

Ni kweli kuwa mwanaume ni kikwazo cha mafanikio katika jamii. Ninathibitisha dai ili kuwa mwanaume ni kikwazo cha mafanikio kwa kutumia riwaya ya TAKADINI na riwaya ya WATOTO WA MAMA NTILIE. Nikianza na riwaya ya WATOTO WA MAMA NTILIE kama ifuatavyo;

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

Mfano - Mzee Lomolomo

Ni mlevi

Mwizi wa mali za familia.

Hahusiki katika malezi ya familia.

RIWAYA YA TAKADINI

Mfano - Mzee Makwati    

Mshikilia mila na desturi potofu

Mwenye ndoa za mitaala

Hana msimamo.

Ni mbaguzi n.k.

Tumia vitabu viwili vya tamthiliya kati ya vilivyoorodheshwa, kujadili madhara ya ukosefu wa elimu katika jamii. Toa hoja tatu kwa kila tamthiliya.

TAMTHILIA YA KILIO CHETU

Mimba za Utotoni - Mfano Suzi anapata mimba katika umri mdogo kutokana na kukosa elimu ya kijinsia.

Maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI- Mfano Joti anaambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa sababu ya kukosa kutoka katika jamii yake.

Mapenzi katika umri mdogo - vilevile ukosefu wa elimu hupelekea kujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo .

TAMTHILIA YA ORODHA

Mmomonyoko wa maadili kwa Watoto- Mfano furaha  anatoloka nyymbani kwa wazazi wake usiku na kwenda bar na rafiki zake.

Maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI- Mfano FURAHA anaambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa sababu ya kukosa kutoka katika jamii yake.

Mapenzi katika umri mdogo - vilevile ukosefu wa elimu hupelekea kujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo . Mfano mhusika Furaha.

 NECTA 2013

“Mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.

Ni kweli kuwa mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii. Ninathibitisha kauli hii kwa kutumia diwani mbili ambazo ni diwani ya WASAKATONGE na diwani ya MALENGA WAPYA. Nikianza na diwani ya WASAKATONGE kama ifuatavyo;

DIWANI YA WASAKATONGE

Mshairi anakemea rushwa - shairi la MVUJA JASHO.

Mshairi anakemea ukeketaji wa mwanamke - Shairi la TOHORA.

Mshairi anakemea Usaliti - Shairi la VINYONGA.

Mshairi anakemea Uongozi mbaya - Shairi la MIAMBA na MADIKTETA.

DIWANI MALENGA WAPYA

Mshairi anakemea uongozi mbaya - Shairi la PUUZO

Mshairi anakemea matabaka - Shairi la PUNDA

Mshairi anakemea matumizi mabaya ya pesa - Shairi la ISRAF

“Fasihi ni chuo cha kufundisha maisha kwa jamii husika. “Jadili ukweli wa kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila riwaya kati ya riwaya mbili ulizosoma.

Ni kweli fasihi ni chuo cha kufundisha maisha kwa jamii husika. Ninathibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutumia riwaya mbili ambazo ni riwaya ya WATOTO WA MAMA NTILIE na riwaya ya TAKADINI . Nikianza na riwaya ya WATOTO WA MAMA NTILIE kama ifuatavyo;

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

Fasihi inafundisha kuwa ulevi si jambo jema. Mfano Mzee Lomolomo.

Fasihi inatufundisha kuwa Watoto wasifukuzwe shule kwa kukosa ada.

Fasihi inatufundisha kuwa rushwa ni adui wa haki.

RIWAYA YA TAKADINI

Fasihi inatufundisha kuwa walemavu wanaweza kufanya mambo makubwa na muhimu katika jamii kama walivyo wengine.

Fasihi inatufundisha kuwa ndoa ni makubaliano ya watu wawili na haipaswi kuingiliwa na mtu yeyote.

Fasihi inatufundisha kuwa baadhi ya mila zilizopitwa na wakati hazifai kuendelea kutumika.

Chagua wahusika watatu wa kike, kutoka katika kila tamthiliya kati ya tamthiliya mbili ulizosoma, kisha onesha kukubalika kwao kama kielelezo cha maisha katika jamii.

(MAMA MAZOEA)

Mlezi mzuri wa familia

Ana ushirikiano mzuri kwa mke mwenzie ma mainda

Mchapakazi

KILIO CHETU (ANNA)

Ana msimamo

Ana mapenzi ya dhati kwa rafiki yake Suzi

Hajihusishi na mapenzi katika umri mdogo.




NECTA 2014

“Ustadi wa msanii hudhihirishwa na fani”. Dhihirisha kauli hiyo kwa kutumia vipengele vitatu vya lugha kwa kila diwani kutoka katika diwani mbili ulizosoma.

Ni kweli kuwa ustadi wa msanii hudhihirishwa na fani. Ninathibitisha  kauli hii kwa kutumia diwani mbili ambazo ni diwani ya WASAKATONGE na diwani ya MALENGA WAPYA. Nikianza na diwani ya MALENGA WAPYA kama ifuatavyo;

DIWANI MALENGA WAPYA

Taswira

Tashibiha

Sitiari

DIWANI WASAKATONGE

Taswira 

Tashibiha

Sitiari

Jadili kukubalika kwa wahusika wawili kama kielelezo halisi cha wanajamii kati ya Takadini, Maman’tilie na Brown Kwacha kutoka katika riwaya mbili ulizosoma. Toa hoja tatu kwa kila mhusika.

RIWAYA YA TAKADINI

Mhusika ni Takadini

Ni mchapakazi

Anapenda kujituma.

Ni mtiifu

Ni jasiri

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

Mhusika ni Mama Ntilie

Ni mchapakazi

Ana mapenzi ya dhati kwa familia yake.

Ni mvumilivu

Ni jasiri

“Kujenga jamii bora ni dhima ya mwandishi.” Thibitisha kauli hii kwa kutumia hoja tatu toka katika kila tamhtiliya kati ya tamthiliya mbili ulizosoma.

Ni kweli kuwa kujenga jamii bora ni dhima ya mwandishi. Ninathibitisha kauli hii kwa kutumia tamthilia mbili ambazo ni NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE pamoja na KILIO CHETU. Nikianza na tamthilia ya NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE kama ifuatavyo; 

TAMTHILIA YA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE

Kupiga vita kuchanganya mapenzi na kazi

Kupiga vita umasikini

Kupiga vita mila potofu/ Ushirikina

Kupiga vita mapenzi ya ulaghai

Kupiga vita ulevi

Kupiga vita uvuvi

TAMTHILIA YA KILIO CHETU

kutetea umuhimu wa elimu ya kijinsia

Kupiga vita mapenzi katika umri mdogo

Kupiga vita mimba za utotoni

Kupiga vita mila potofu

Kupiga vita athari za utandawazi katika jamii

 NECTA 2015

"Kazi za fasihi hufichua mivutano iliyopo katika jamii." Kwa kutumia hoja tatu kwa kila diwani fafanua mivutano hiyo kutoka katika diwani mbili ulizosoma.

"Mandhari iketeuliwa vizuri humsaidia mwandishi katika kufikisha yale aliyokusudia kwa jamii yake" Thibitisha hoja hiyo kwa kutoa mifano mitatu toka katika kila kitabu kati ya riwaya mbili zilizoorodheshwa.

Kwa kutumia tamthiliya mbili miongoni mwa zilizoorodheshwa eleza jinsi waandishi walivyoonesha athari za utamaduni wa kigeni katika maadili ya jamii ya kiafrika.

NECTA 2016

"Mshairi ni mwalimu wa viongozi wa nchi." Jadili kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.

DIWANI YA MALENGA WAPYA

Mshairi kufundisha kuhusu matabaka - Katika Shairi la PUNDA.

Mshairi kufundisha kuhusu matumizi mazuri ya pesa - Katika Shairi la ISRAF

Mshairi kufundisha kuhusu uongozi mbaya - Katika Shairi la PUUZO

Mshairi kufundisha kuhusu umuhimu wa kilimo Katika Shairi la ADUI

DIWANI YA WASAKATONGE

Mshairi kufundisha kuhusu usaliti kwa viongozi - Katika shairi la VINYONGA

Mshairi kufundisha kuhusu matabaka katika jamii - Katika Shairi la WASAKATONGE

Mshairi anafundisha kuhusu uongozi mbaya - Katika shairi la MIAMBA

Mshairi anafundisha kuhusu Ukoloni Mambo Leo - Katika Shairi la BUNDI

 "Fasihi ya Kiswahili imemweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti." Thibitisha usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

Mwanamke amewekwa kama mlezi wa familia- Mama NTILIE

Mwanamke amewekwa kama mtu mwenye huruma na moyo wa kutoa msaada. Zenabu.

Mwanamke amewekwa kama mtu mwenye uvumilivu na upendo- Mama Ntilie.

RIWAYA YA TAKADINI

Mwanamke amewekwa kama mwanamapinduzi - Sekai na Shanghai

Mwanamke amewekwa kama jasiri - Sekai

Mwanamke amewekwa kama mtu mwenye mapenzi ya dhati- Sekai na shinghai.

Kwa kutumia hoja tatu kwa kila tamthiliya kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma, jadili kufaulu kwa waandishi katika kipengele cha utumizi wa tamthali za semi.

 NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE

Tashibiha > suruali kama kengele ya bomani

Takriri> jamani! Jamani!

Mdokezo > sijui..siwezi

 KILIO CHETU

Takriri> watu walipukutika, wakapukutika

Mdokezo> Joti..

Tashibiha> wakapukutika kama majani kiangazi

Misimu> Joti mshashi.


NECTA 2017

“Msanii ni kinda la jamii husika hivyo anayoandika huihusu jamii hiyo.” Jadili kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.

“Elimu ni ufunguo wa maisha.” Fafanua kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kati ya vitabu viwili vya riwaya vilivyoorodheshwa.

“Washairi hutumia mashairi yao kuelimisha jamii kuhusu mambo yanayoikabili.” Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.

UTANGULIZI

Ni kweli kuwa washairi hutumia mashairi yao kuelimisha jamii kuhusu mambo yanayoikabili. Ninathibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutumia  diwani mbili ambazo ni DIWANI YA WASAKATONGE na DIWANI YA MALENGA WAPYA. Nikianza na DIWANI YA WASAKATONGE kama ifuatavyo;

WASAKATONGE

Kuelimisha kuhusu uongozi mbaya  katika Shairi la “MADIKTETA” “UNYAMA”

Kuelimisha kuhusu ukoloni mambo leo  katika Shairi la “KLABU” BUNDI“

Kuelimisha kuhusu uwepo wa  matabaka  katika Shairi la “MVUJA JASHO” “WALALA HOI”

Kuelimisha kuhusu usaliti kwa viongozi - katika Shairi la   “VINYONGA”

Kuelimisha kuhusu ukeketaji wa wanawake - Katika Shairi la "TOHARA"

MALENGA WAPYA

Kuelimisha kuhusu matabaka -  Katika Shairi la “SAMAKI MTUNGONI” “PUNDA”

Kuelimisha kuhusu uongozi mbaya -  Katika Shairi la “PUUZO” “BAHARI’ n.k

Kuelimisha kuhusu unyonyaji -  Katika Shairi la “BAHARI” “SAMAKI MTUNGONI” “ HALI HALISI”

Kuelimisha kuhusu Umuhimu wa kutumia pesa vizuri - Katika Shairi la  “ISRAFU

NECTA 2018

“Mwanamke ni mtu mwenye huruma na fadhila.” Thibitisha hoja hiyo kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika vitabu viwili vya riwaya kati ya vilivyoorodheshwa.

Ni kweli mwanamke ni mtu mwenye huruma na fadhila. Ninathibitisha hoja hiyo kwa kutumiavitabu viwili vya riwaya ambazo ni riwaya TAKADINI pamoja na riwaya WATOTO WA MAMA NTILIE. Nikiamza na riwaya ya TAKADINI kama ifuatavyo;

RIWAYA YA TAKADINI

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

“Waandishi wa tamthiliya wameshindwa kufikisha ujumbe kwa jamii iliyokusudiwa.” Kanusha kauli hii kwa kutumia hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma.

Si kweli kuwa waandishi wa tamthiliya wameshindwa kufikisha ujumbe kwa jamii iliyokusudiwa. Ninakanusha kauli hii kwa kutumia tamthilia mbili ambazo ni KILIO CHETU pamoja na NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE. Nikianza na tamthilia ya KILIO CHETU kama ifuatavyo; 

TAMTHILIA YA KILIO CHETU

TAMTHILIA YA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE.

Washairi hutumia mashairi yao kuelimisha jamii kuhusu mambo yanayoikabili. Tbitisha ukweli wa kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika diwani mbili ulizosoma.

WASAKATONGE

1.Kuelimisha kuhusu uongozi mbaya  katika Shairi la “MADIKTETA” “UNYAMA”

2.Kuelimisha kuhusu ukoloni mambo leo  katika Shairi la “KLABU” BUNDI“

3.Kuelimisha kuhusu uwepo wa  matabaka  katika Shairi la “MVUJA JASHO” “WALALA HOI”

Kuelimisha kuhusu usaliti kwa viongozi - katika Shairi la   “VINYONGA”

Kuelimisha kuhusu ukeketaji wa wanawake - Katika Shairi la "TOHARA"

MALENGA WAPYA

Kuelimisha kuhusu matabaka -  Katika Shairi la “SAMAKI MTUNGONI” “PUNDA”

Kuelimisha kuhusu uongozi mbaya -  Katika Shairi la “PUUZO” “BAHARI’ n.k

Kuelimisha kuhusu unyonyaji -  Katika Shairi la “BAHARI” “SAMAKI MTUNGONI” “ HALI HALISI”

Kuelimisha kuhusu Umuhimu wa kutumia pesa vizuri - Katika Shairi la  “ISRAFU”

NECTA 2019

Kwa kutumia diwani mbili ulizosoma, eleza jinsi taswira tatu kutoka katika kila diwani zilivyotumiwa na msanii kuwasilisha ujumbe kwa jamii.

Diwani ya wasakatonge  

Taswira ya Vinyonga - Ujumbe "Viongozi wasaliti mwenye tabia ya kigeugeu. Katika shairi la VINYONGA.

Taswira ya Miamba - Ujumbe " Watu mwenye mamlaka /watu wa tabaka la juu au wenye dhamana. Katika shairi la MIAMBA.

Taswira ya Bundi - Ujumbe " wakoloni mamboleo" katika shairi la BUNDI.

Taswira ya Jiko - Ujumbe " Mwanamke asiyejitunza na kujieheshimu yaani Malaya . katika shairi la WEWE JIKO LA SHAMBA.

Taswira ya Wasakatonge - Ujumbe " Watu wa Tabaka la chini ( Masikini) katika Shairi la WASAKATONGE.

Taswira ya Tonge la ugali - Ujumbe " Malighafi" katika shairi la Tonge la Ugali.

DIWANI YA MALENGA WAPYA

Taswira ya njiwa - Ujumbe  " Mpenzi " Shairi la NIPATE WAPI MWINGINE?

Taswira ya Punda - Ujumbe " tabaka linalokandamizwa " shairi la PUNDA.

Taswira la UA - Ujumbe " Mwanamke" Shairi la UA.

Taswira ya Samaki - Ujumbe " Tabaka tawaliwa au mwanachi wa tabaka la chini" Shairi la SAMAKI MTUNGONI.

Taswira ya Mvuvi - Ujumbe " Ni watu wa tabaka la juu (viongozi ) shairi la SAMAKI MTUNGONI.

Taswira ya MTUNGO - Ujumbe " Ni sheria ,kanuni au taratibu zinazotumiwa kuwabana watu wa tabaka la chini. Shairi la SAMAKI MTUNGONI.

“Waandishi wa kazi za fasihi huibua migogoro mbalimbali na kupendekeza masuluhisho ili kuelimisha jamii husika”. Thibitisha kauli hiyo kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.

Ni kweli kuwa waandishi wa kazi za fasihi huibua migogoro mbalimbali na kupendekeza masuluhisho ili kuelimisha jamii husika. Ninathibitisha kauli hiyo kwa kutumia riwaya ya TAKADINI pamoja na WATOTO WA MAMA NTILIE. Nikianza na riwaya ya TAKADINI kama ifuatavyo;

RIWAYA YA TAKADINI

Mgogoro wa makwati na  - Suluhisho la mgogoro sekai aliamua kutoroka kijijini ili kunusuru maisha ya mtoto Takadini.

Mgogoro wa shingai na wazazi wake - suluhishoe lake shinghai anaamua kutorokea kwa Takadini.

Mgogoro wa sekai na jamii yake - suluhisho lake sekai aliamua kutoroka kijijini ili kunusuru maisha ya mtoto Takadini.

RIWAYA YA MAMANTILIE

Mwalimu Chikoya na Mwanafunzi wasiokuwa na ada wala safe za shule - Suluhisho lake ni Mwanafunzi nao kufukuzwa shule.

Mama ntilie na mzee Lomolomo - Suluhisho ni kifo cha mzee Lomolomo.

Peter na Doto. Suluhisho la mgogoro huu ni kurwa kumsaidia Peter.

Kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma, fafanua madhara yanayotokana na kukosekana kwa elimu ya jinsia kwa vijana kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila kitabu.

TAMTHILIA YA KILIO CHETU

Mimba za Utotoni - Mfano Suzi anapata mimba katika umri mdogo kutokana na kukosa elimu ya kijinsia.

Maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI- Mfano Joti anaambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa sababu ya kukosa kutoka katika jamii yake.

Mapenzi katika umri mdogo - vilevile ukosefu wa elimu hupelekea kujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo .

TAMTHILIA YA ORODHA

Mmomonyoko wa maadili kwa Watoto- Mfano furaha  anatoloka nyymbani kwa wazazi wake usiku na kwenda bar na rafiki zake.

Maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI- Mfano FURAHA anaambukizwa ugonjwa wa zinaa kwa sababu ya kukosa kutoka katika jamii yake.

Mapenzi katika umri mdogo - vilevile ukosefu wa elimu hupelekea kujiingiza katika mapenzi katika umri mdogo . Mfano mhusika Furaha.





NECTA 2020

Kauli za washairi ni nyenzo muhimu katika ujenzi wa jamii bora. Thibitisha usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika diwani mbili ulizozisoma.

Ni kweli kuwa kauli za washairi ni nyenzo muhimu katika ujenzi wa jamii bora. Ninathibitisha usemi huu kwa kutumia diwani mbili ambazo ni WASAKATONGE na diwani ya MALENGA WAPYA. Nikianza na diwani ya WASAKATONGE kama ifuatavyo; 

WASAKATONGE

Kupiga vita uongozi mbaya “madikteta” “unyama”

Kupiga vita ukoloni mambo leo “klabu” “hatuna kauli”

Kupiga vita matabaka “mvuja jasho” “walala hoi”

Kuwa na demokrasia ya kweli na utu ‘Saddam Hussein” “madikteta”

MALENGA WAPYA

Kupiga vita matabaka “Samaki mtungoni” “punda”

Kupiga vita uongozi mbaya “puuzo” “bahari’ n.k

Kupiga vita unyonyaji “Bahari” “Samaki” “ Hali halisi”

Umuhimu wa kutumia pesa vizuri “Israfu”

“Jamii ya kitanzania inakabiliwa na matatizo mbalimbali ya kijamii yanayokwamisha maendeleo.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila riwaya kati ya riwaya mbili ulizosoma.

Ni kweli kuwa jamii ya kitanzania inakabiliwa na matatizo mbalimbali ya kijamii yanayokwamisha maendeleo. Ninathibitisha kauli hii kwa kutumia riwaya mbili ambazo ni TAKADINI na WATOTO WA MAMA NTILIE. Nikianza na riwaya ya TAKADINI kama ifuatavyo; 

RIAWAYA YA TAKADINI

Dhana potofu ya kuamini vitu visivyo na msingi.

Ndoa za .

Umasikini.

Ubaguzi na unyanyasaji.

RIWAYA YA WATOTO WA MAMA NTILIE

Umaskini.

Ukosefu wa elimu.

Wizi na ujambazi.

Rushwa.

Watoto wa mitaani.

“Waandishi wa kazi ya fasihi hulenga kuleta mabadiliko katika yale wanayoyaandika.” Kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma, tetea kauli hii kwa kutumia hoja tatu kutoka katika kila kitabu.

Ni kweli kuwa waandishi wa kazi ya fasihi hulenga kuleta mabadiliko katika yale wanayoyaandika. Ninathibitisha kwa kutumia tamthiliya mbili kati ya NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE na KILIO CHETU. Nikianza na tamthilia ya NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE kama ifuatavyo;

TAMTHILIA YA NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE

Kupiga vita kuchanganya mapenzi na kazi

Kupiga vita umasikini

Kupiga vita mila potofu/ Ushirikina

Kupiga vita mapenzi ya ulaghai

Kupiga vita ulevi

Kupiga vita uvuvi

TAMTHILIA YA KILIO CHETU

kutetea umuhimu wa elimu ya kijinsia

Kupiga vita mapenzi katika umri mdogo

Kupiga vita mimba za utotoni

Kupiga vita mila potofu

Kupiga vita athari za utandawazi 



No comments:

Post a Comment

Maswali ya vitabu na majibu yake

 NECTA 2012 “Washairi ni wataalamu wazuri na waliobobea katika kutumia taswira zinazotoa ujumbe kwa jamii.” Tumia taswira tatu kwa kila diwa...